I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, May 23, 2010

ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Amani Abeid Karume ameondoka nchini kuelekea China kwa ziara maalum ya wiki moja.
Akiwa nchini humo rasi Karume athudhuria maonyenyesho ya biashara ya Kimataifa yatakayofanyika mjini Shanghai China.
Katika ziara yake hiyo Rais Karume anafuatana na mkewe Mama Shadya Karume na viongozi na maafisa wengine wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
Miongoni mwa viongozi hao ni waziri wa Utalii, Biashara na uwekezaji Samia Suluhu Hassan, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Seif Ali Iddi na viongozi wengine wa serikali zote mbili.
Mara baada ya kumaliza ziara ya wiki moja ya nchini China, Rais Karume anatarajia kwenda nchini Qatar kwa ajili ya kuhudhuria mkutano Mkuu wa Kiuchumi Duniani utakaofanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo Doha.

No comments:

Post a Comment