I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, May 9, 2010

MAALIM SEIF ATANGAZA NIA YAKE YA KUGOMBEA TENA URAIS


Katibu mkuu wa chama cha wananchi CUF, Seif Sharif Hamad ametangaza nia yake ya kugombea tena nafasi ya urais wa Zanzibar kwa mara ya nne katika uchaguzi mkuu ujao mwaka huu.
Hatua hiyo ya Hamad kutangaza kugombea nafasi hiyo imekuja siku moja baada ya mwenyekiti wa chama hicho taifa Profisa Ibrahim Harouna Lipumba kutangaza kugombea nafasi ya urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama hicho.
Katibu mkuu huyo ameweka bayana nia yake hiyo ya kugombea nafasi ya urais wa Zanzibar ikiwa imebakia miezi mitano kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar
Uchaguzi mkuu wa Zanzibar utakao wachaguwa madiwani, wawakilishi na rais wa Zanzibar unatarajiwa kufanyika Octoba 31 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment