I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, May 27, 2010

DAR ES SALAAM:

Chama cha jamii C.C.J kimesema kiko tayari kutoa fedha ili kuharakisha mpango wa unaotakiwa kufanywa na afisi ya msajili ya vyama vya siasa nchini ili kukiwezesha chama hicho kupata usajili wa kudumu na kushiriki katika uchaguzi mkuu wa Octoba mwaka huu.
Kauli hiyo imetolewa na Msemaji wa chama hicho Fedrick Mpendazoe mjini Dar es Salaam ambae amepinga kile inachodaiwa hujuma zinazofanywa na msajili wa vyama vya siasa nchini John Tendwa dhidi ya chama hicho.
Hata hivyo Tendwa amesema hakuna utaratibu wa chama kuharakisha mpango unatakiwa kufanywa na afisi ya msajili wa vyama vya siasa ili kukiwezesha chama kupata usajili wa kudumu.

No comments:

Post a Comment