I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, April 29, 2010

AMETUMIA SHOKA KWA KUWAUWA WATOTO WAKE WATATU

Mwanamke mmoja katika mkoa wa Kilimanjaro ametumia shoka kwa kuwauwa watoto wake watatu na mmoja kumjeruhi usiku wa kumkia jana.

Tukio hilo limeibua simanzi miongoni mwa wakaazi wa eneo hilo ambao wamedai mwanamke huyo ni mgonjwa wa akili amekuwa na mvutano na mumewe mara kwa mara na anashikiliwa na jeshi la polisi.

Wakizungumzia tukio hilo baadhi ya majirani wa familia hiyo wamesema kitendo hicho ni ukatili na mwanamke huyo alikuwa akinywa pombe na wakati mwengine alikuwa akichanganyikiwa na kuzungumza mambo yasioeleweka.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kilimanjaro Lukas Ngoboko amesema miongoni mwa watoto waliouwawa katika tukio hilo ni mlemavu wa viungo asiekuwa na akili na mtoto aliejeruhiwa amelazwa hospitali akiwa na hali mbay

No comments:

Post a Comment