I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, April 14, 2010

WATOTO WENYE ULEMAVU ZANZIBAR


Watoto wengi wenye ulemavu Zanzibar wanakabiliwa na matatizo kutokana na huduma za watu wenye ulemavu kutopewa umuhimu katika mipango na bajeti za wizara za serikali.
Mkurugenzi wa mradi wa marekebisho ya watoto wenye ulemavu Tala Mswalam Said amesema vijana wenye ulemavu wanakosa visaidiza vya kufanya shughuli muhimu za kijamii kutokana na serikali kutolipa umuhimu suala hilo..
Akifungua semina juu ya mahitaji ya marekebisho ya watu wenye ulemavu mjini hapa amesema visaidizi ni nyenzo muhimu kwa vijana wenye ulemavu zitakazowasaidia katika shughuli zao za maendeleo.
Amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoridhia mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu ambao unazitaka nchi hizo kuweka mikakati ya kuwawezesha watu wenye ulemavu kushiriki katika kujiletea maendeleo.

Hivyo amesema iko haja kwa serikali kutenga bajeti maalum kwa ajili ya kuwaendeleza watu wenye ulemavu hasa katika masuala ya kuwapatia ajira.
Nae waziri wa nchi afisi ya waziri kiongozi Hamza Hassan Juma akifungua semina hiyo amewataka wakuu wa taasisi za serikali kuzingatia mahitaji ya watu wenye ulemavu wanapoandaa mipango ya taasi zao.
Amesema serikali imeandaa sera na sheria za kuwalinda watu wenye ulemavu ili kuona kundi hilo linashiriki katika sekta zote za jamii na uchumi hasa katika suala la kupatiwa ajira.
Semina hiyo ya siku mbili imeandaliwa na taasisi ya Civil Society na kuhudhuriwa na wakuu wa baadhi ya taasisi za serikali na jumuiya za kiraia.

No comments:

Post a Comment