I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, April 26, 2010

RAIS WA TANZANIA JAKAYA MRISHO KIKWETE AMETOA MSAMAHA KWA WAFUNGWA ELFU TATU 101 KATIKA KUADHIMISHA MIAKA 46 YA MUUNGANO.


Rais wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete ametoa msamaha kwa wafungwa elfu tatu 101 katika kuadhimisha miaka 46 ya muungano.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kutiwa saini na waziri wa mambo ya ndani Laurent Masha imesema msamaha huo unawahusu wafungwa wanaotumikia kifungo kisichozidi miaka mitano, wenye magonjwa kama vile ukimwi, kifua kikuu na saratani.
Msamaha huo pia utawahusu wafungwa wazee kuanzia miaka 70, wafungwa wa wakike waliofungwa wakiwa wajawazito, walioingia kifungoni wakiwa na watoto wachanga na wenye ulemavu wa mwili na akili.
Aidha mshamaha huo wa rais hautawahusu wafungwa waliohukumiwa kunyongwa na adhabu hiyo itabadilishwa kuwa kifungo na wafungwa waliohukumiwa kifungo cha maisha.
Wafungwa wengine ni wale wanaotumikia kifungo cha dawa za kulevya, rushwa, kunyanganya na kutumia silaha pamoja na wafungwa wanaotumikia kifungo cha kupatikana na silaha.
Wafungwa wengine amabao hauhusiki na msamaha huo wanaotumikia kifungo kwa makosa ya kujamiana, waliowapa ujauzito wanafunzi wa skuli za misingi, wizi wa miundo mbinu na wale waliotoroka chini ya ulinzi.

Wakati huo huo Viongozi wa dini nchini wamewaombea dua watanzania kujiepusha na siasa za kidini, ukabila, chuki na ueneo ili uchaguzi wa mwaka huu ufanyike kwa amani, haki na uhuru.
Wakiomba dua katika sherehe za maadhimisho ya miaka 46 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar mjini Dar es Salaam wamesema siasa za aina hiyo zinaweza kuvuruga amani na umoja wa Tanzania.
Kiongozi kutoka dini ya Kislamu Alhaji Mussa Salum amesema watanzania wanaendelea kufaidika na matunda ya muungano na kumuomba mwenyezi Mungu uchaguzi mkuu ujao ufanyike kwa amani na utulivu …
Nae askofu Sastari Lebena na Steven Manana wamesema wakati huu Tanzania inapoadhimisha miaka 46 ya muungano na kuelekea katika kipindi cha uchaguzi mkuu amewaombea watanzania kuwa na uvumilivi ili kuchagua viongozi wenye uchungu na nchi yao…
Uongozi wa Zenji fm radio na wafanyakazi wake inawatakia kila la kheir watanzania wote katika kuadhimisha miaka 46 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

No comments:

Post a Comment