I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, April 14, 2010

WASOMALI WAENDELEZA WIMBI LA UTEKAJI NYARA MELI


MOGADISHU:
Maharamia wa Somalia wameiteka nyara meli ya Umoja wa Falme za Kiarabu ikiwa na mabaharia 26 karibu na visiwa vya Ushelisheli iliyokuwa ikija hapa Zanzibar.
Mabaharia 10 kati ya waliomo kwenye meli hiyo ni raia wa Tanzania, 11 ni raia wa India na watano ni raia wa Pakistan.
Habari zinasema kwamba maharamia hao wameipeleka meli hiyo kwenye fukwe za Somalia.
Maafisa wa safari za baharini wa India wamesema kwamba katika kipindi cha wiki mbili zilizopita, maharamia wa Somalia wameteka meli 11 ambapo mabaharia 120 wa India ni miongoni mwa watu waliokuwemo kwenye meli hizo.
Takwimu za kimataifa zinaonesha kuwa idadi ya mashambulizi ya maharamia wa Somalia katika bahari ya Hindi na Ghuba ya Aden yaliongezeka sana mwaka uliopita wa 2009 ikilinganishwa na mwaka 2008.

1 comment:

  1. kiasi yaongezeke . Ajira kwa wasomali ni tatizo .

    ReplyDelete