I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, April 29, 2010

MUANDISHI ZNZ ATUMIWA SMS ZA VITISHO


Mwaandishi mwandamizi anaefanyia kazi katika kampuni ya IPP media Maulid Hamad Maulid ameelezea kutumiwa ujumbe mfupi wa vitisho katika simu yake ya mkononi unaohatarishan maisha.
Akizungumza na waandishi wa habari huko idara ya habari Zanzibar amesema ujumbe huo ametumiwa baada ya kutoa taarifa zinazohusiana na migogoro ya ardhi ambayo inatokea katika kisiwa cha Unguja ambayo inaathiri kundi kubwa la wananchi.
Amesema kutokana na hali hiyo tayari amesehatoa taarifa kwa jeshi la polisi na mkurugenzi wa upelelezi na kuahidi suala mwa mwandishi huyo watalifanyia kazi.
Maulid Hamadi amekuwa akitoa taarifa ya Migogoro ya ardhi katika maeneo mbali mbali ikiwemo, Muyuni C, Kijiji cha Pwani mchangani, msitu wa hifadhi Kibuteni, Bumbwini Kiongwe pamoja na Fuoni Kibondeni.

No comments:

Post a Comment