I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, April 15, 2010

TUTENGENEZEWEE SEHEM MAALUM YA SOKO LETU


Umoja wa watu wenye ulemavu Zanzibar umelitaka baraza la manispaa Zanzibar kutenga sehemu katika soko la mwanakwerekwe na eneo la biashara la Saateni ili kuwawezesha watu wenye ulemavu kufanya biashara katika maeneo hayo.
Akizungumza na Zenji Fm Radio mkuu wa mipango wa umoja huo Salma Haji Saadat amesema hali iliyopo sasa katika sehemu hizo haitoi nafasi kwa watu wenye ulemavu kufanya biashara.
Amesema watu wenye ulemavu wamehamasika kufanya biashara ili kuondokana na utegemezi katika familia zao, lakini baadhi ya taasisi hazingatii mahitaji ya watu hao katika mipango yao ya kiuchumi.
Amesema kwa mujibu wa sheria namba tisa ya kulinda haki za watu wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na kujiendeleza kiuchumi, sheria hiyo bado haijatekelezwa kikamilifu kutokana na kutokuwepo sehumu zenye kutoa huduma kwa watu maalum

No comments:

Post a Comment