I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, April 12, 2010

VITAMBULISHO VYA UKAZI VYALETA UTATA ZANZIBAR

Afisi ya vitambulisho vya ukaazi imelalamikiwa na baadhi ya masheha kwa kuwapatia vitambulisho vya mzanzibari mkaazi wananchi bila kupatiwa fomu kutoka kwa masheha.
Malalamiko hayo yamejitokeza katika baadhi ya vituo vya uandikishaji vya majimbo ya Kwamtipura, Chumbuni na Amani baada ya badhi ya vijana kunyanganywa vitambulisho vyao na masheha kwa madai ya kuvipata kwa udanganyifu.
Sheha wa shehia ya Kwamtipura, Machano Salum Khamis amesema wananchi wanaomba vitambulisho vya ukaazi hupatiwa barua za masheha, lakini hivi sasa wanaomba moja kwa moja katika afisi ya vitambulisho.
Amesema hali hiyo imekuwa ikisababisha udanganyifu na hivyo amechukua uwamuzi wa kuwanyanganya vitambulisho hivyo baadhi ya vijana waliokwenda kujiandikisha kwa madai ya kivipata visivyo halali.

Hata hivyo vijana wengine walirudishiwa vitambulisho vyao baada ya kufika afisini kwake
Kazi za undikishaji zinaendelea katika majimbo ya Rahaleo, Mjimkongwe na Kikwajuni baada ya kumalizika jana katika majimbo ya Chumbuni, Kwamtipura na Amani.
Hata hivyo kazi hizo za uandikshaji katika majimbo hayo zimekumbwa na tatizo la wananchi kutojua mipaka ya majimbo yao na kusababishwa kukataliwa kuandikishwa katika daftari la wapiga kura.
Kwa mujibu wa tume ya uchaguzi Zanzibar zaidi ya watu laki tatu na elfu 65 wameandikishwa katika daftari la kupiga kura katika maeneo mbali mbali ya Unguja na Pemba.
Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni afisa wa habari wa tume hiyo Idrissa Haji Jecha amesema idadi kubwa ya watu wamejitokeza kujiandikisha katika awamu ya pili inayomalizia katika baadhi ya majimbo.

No comments:

Post a Comment