I made this widget at MyFlashFetish.com.

Saturday, April 24, 2010

TUME YA UCHAGUZI ZENJI YAONGEZA DHAMANA KWA WAGOMBEA KITI CHA URAIS KATIKA UCHAGUZI WA 2010


ZANZIBAR:

Tume ya uchaguzi Zanzibar imepandisha dhamana ya wagombea wa kiti cha urais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Octoba mwaka huu kutoka shilingi milioni moja hadi milioni tatu.

Akizungumza na Zenji Fm radio juu ya ratiba ya uchaguzi mkuu, afisa habari wa tume hiyo Idriss Haji Jecha amesema kiwango hicho kimeongezwa kutokana na hali ya kifedha ya watu wanaotaka kugombania urais na kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania.

Aidha tume hiyo pia imepandisha dhamana kwa nafasi za uwakilishi kutoka shilingi elfu 50 hadi laki tatu na nafasi za udiwani kutoka shilingi elfu 15 hadi shilingi elfu 50

Kwa mujibu wa taarifa ya tume hiyo uteuzi wa wagombea kwa nafasi zote tatu utafanyika tarehe 03 Septemba ambao utatanguliwa na uchukuwaji wa fomu utakaonza tarehe 10 hadi tarehe 30 Agosti.

Kampeni za wagombea zitaanza tarehe 10 Septemba hadi tarehe 30 Octoba ambapo vyama vitakavyoweka wagombea wa nafasi ya urais wa Zanzibar vitawasilisha ratiba zao za kampeni kwa tume hiyo si zaidi ya tarehe 30 Agosti.

Aidha tume ya uchaguzi imesema upigaji kura utafanyika siku ya Jumapili ya tarehe 31 Octoba na matokeo ya uchaguzi yanatarajiwa kutangazwa kuanzia tarehe 31 hadi tarehe 02 Octoba

No comments:

Post a Comment