I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, April 8, 2010

UMEME ZANZIBAR BADO TATIZO


Serikali ya mapinduzi Zanzibar imesema hali ya umeme katika kisiwa cha Unguja bado sio nzuri licha ya matengenezo makubwa yaliofanywa hivi karibuni baada ya huduma hiyo kukatika kwa kipindi cha miezi mitatau.
Waziri wa maji ujenzi, nishati na ardhi Mansour Yussuf Himid amesema ili kuepukana na hali hiyo amewataka wananchi kupunguza matumizi ya umeme yasio kuwa ya lazima.
Amesema serikali inaendelea na juhudi za kupata uemem wa hakiba ili kukabiliana na tatizo hilo na kusema kazi za ujenzi wa kuweka majenerata ya kuzalisha umeme wa dharura zinaendelea katika eneo la Mtoni.
Amesema majenerata hayo yanayotarajiwa kuwasili nchini hivi karibuni yatakidhi mahitaji ya umeme kwa asilimia 50 Akizungumzia mradi wa kuweka waya mpya wa umeme unaofadhiliwa na serikali ya Marekani waziri Mansour amesema mkandarasi wa ujenzi huo ameshapatikana na utiaji wa saini unatarajiwa kufanyika mwezi uajao kwa ajili ya utengenezaji wa waya huo na kulazwa.
Hata hivyo waziri Mansour amewataka wananchi kutojenga katika eneo linalopita mdaradi huo ili ujenzi wa mradi huo usichelewe

No comments:

Post a Comment