I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, April 28, 2010

KITENGO CHA KICHOCHO,MATENDE NA MINYOOO ZANZIBAR KIMESEMA UGONJWA WA MATENDE ZANZIBAR UMEWEZA KUPUNGUA CHINI YA ASILIMIA MOJA


Kitengo cha kichocho,matende na minyooo Zanzibar kimesema ugonjwa wa matende Zanzibar umeweza kupungua chini ya asilimia moja ya vimelea katika miili ya wagonjwa wanaougua hapa Zanzibar.
Akizungumza na zenji fm radio Meneja wa kitengo hicho Dr.Khalfan Abdallah Mohammed amesema mafanikio hayo yamekuja kutokana na jitihada kubwa walizozichukua ikiwa pamoja na ugawaji wa dawa kila mwaka katika wilaya mbali mbali za Zanzibar.
Amesema mbali ya ugawaji wa dawa elimu mbali mbali zimekuwa zikitolewa kwa wananchi juu kufahamu dalili za ugonjwa huo na kufika vituo vya afya kwa kupata matibabu muafaka.
Ameyataja maeneo yayoathirika zaidi na ugonjwa huo kuwa ni Mkoa wa kusini Unguja na Mkoa wa kusini Pemba…).
Amesema kutokana na mafanikio hayo kitengo hicho hivi sasa wataendeleza uchunguzi kwa kila mwaka kuangalia hali inaendeleaje sambamba na kuwashughulikia wale ambao wameathirika na ugonjwa huo.
Aidha ameitaka jamii kuondokana na imani potofu kwamba ugonjwa huo ni waurithi na baadala yake ugonjwa amesema ugonjwa huo unatonakana na kuenezwa na mbuu

No comments:

Post a Comment