I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, April 12, 2010

CUF IMESEMA ZAIDI YA WANANCHI MIA MBILI NA 82 WAMEKATALIWA KUANDIKISHWA KATIKA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI KUTOKANA NA UTASHI WA KISIASA.


Chama cha wananchi CUF kimesema zaidi ya wananchi mia mbili na 82 katika majimbo ya Dimani, Magogoni na Mwanakwerekwe wamekataliwa kuandikishwa katika daftari la wapiga kura awamu ya pili kutokana na utashi wa kisiasa.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa CUF Juma Said Sanani amedai wananchi hao wanavyo vielelezo vyote vinavyowaruhusu kuandikishwa, lakini wamekosehwa haki yao hiyo ya kidemokrasia.
Akizungumza na Zenji Fm radio amesema miongoni mwao ni mia moja na 85 kutoka jimbo la Dimani, 36 jimbo la Magogoni na 43 jimbo la Mwanakwerekwe.
Aidha amedai masheha ambao ni wakala wa tume ya uchaguzi ndio waliopinga kuandikishwa kwa watu hao kwa kile alichodai kutokana na itikadi zao za kisaisa
Kazi za uandikishaji katika daftari la wapiga kura awamu ya pili hivi sasa zinaendelea katika majimbo ya Rahaleo na Kikwajuni wilaya ya mjini

No comments:

Post a Comment