I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, April 28, 2010

WAISLAM ZANZIBAR KUANDAMANA


Jumuiya ya uamsho na mihadhara ya kiislamu Zanzibar inatarajia kufanya Maandamano makubwa yenye lengo la kupinga uvunjaji wa minara ya miskiti nchini Uswiss .
Akizungumza na zenji Fm radio katibu wa jumuiya hiyo Sheikh Abdalla Saidi amesema maandamano hayo yanatarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa tarehe 30.04.2010 ambayo yataanzia Masjid Mbuyuni baada ya sala ya Ijumaa kupitia kinazini na kuishia viwanja vya Lumumba.
Amesema maandamano hayo ni muhimu kwa vile huu ni wakati ambao waislamu wanatakiwa kuonyesha umoja wao kwa kupinga udhalilishaji dhidi ya dini yao……
Sheik Abdallah ametoa Wito kwa waislamu kushiriki kikamilifu katika pinga suala hilo ambalo limekuwa likidhalilisha uislamu kwa miaka mingi.

No comments:

Post a Comment