I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, April 27, 2010

MAREKANI KUISAIDA ZANZIBAR KATIKA MRADI WA WAYA MPYA WA UMEME WA MEGAWATI 100


Marekani imesema itaendelea kuunga mkono mpango wa nishati wa Zanzibar kwa kusaidia mradi wa waya mpya wa umeme wa Megawati 100 kupitia shirika la nchi hiyo la changamoto la Mellenium.
Balozi wa Marekani nchini Tanzania Alfonso Lenna amesema mkataba wa mradi huo wa kuweka waya wa kupitishia umeme kutoka Tanzania bara unatarajiwa kutiwa saini mwishoni mwa wiki hii.
Akizungumza na rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa bartaza la Mapinduzi Dr. Amani Abeid Karume balozi Lenna amesema mradi huo ni mkubwa kuwahi kufadhiliwa na shirika la Changamoto la Marekani.
Amesema waya huo wa aina yake utatengenezwa nchini Japan na utumika kwa muda mrefu yakiwemo matumizi ya mawasiliano ya Internet ambayo yatasaidia kuchangia maendeleo ya uchumi wa Zanzibar.
Nae rais Karume emeishukuru serikali ya Marekeni kupitia shirika la Changamoto kwa ufadhi wa mradi huo ambao utasaidia maendeleo ya kiuchumi Zanzibar.
Hivi karibuni waziri wa maji, ujenzi, nishati na ardhi Mansour Yussuf Himid amesema kisiwa cha Unguja bado kinakabiliwa na tatizo la umeme licha ya matengenezo makubwa yalifanywa kwenye waya wa sasa unaoleta umeme kutoka Tanzania bara.
Amesema waya huo wa megawati 45 licha ya kumalizika kwa muda wake, umezidiwa na matumizi na kuwataka wananchi kujiepusha na matumizi yasiokuwa ya lazima.

No comments:

Post a Comment