I made this widget at MyFlashFetish.com.

Friday, April 9, 2010

MAHAKAMA YA RUFAA TANZANIA IMEKAMILISHA UWASILISHAJI WA HOJA ZA PANDE MBILI DHIDI YA RUFAA YA SERIKALI YA KUPINGA UWAMUZI WA MAHAKAMA KUU

Mahakama ya rufaa Tanzania imekamilisha uwasilishaji wa hoja za pande mbili dhidi ya rufaa ya serikali ya kupinga uwamuzi wa mahakama kuu kutowa uwamuzi wa kuruhusu mgombea binafsi katika uchaguzi.
Kesi hiyo ilifunguliwa na mwenyekiti wa chama cha Democratic Party Mchungaji Chstopher Mtikila ambae amesema uwamuzi wa rufaa hiyo utakuwa wa kihistoria katika mustakabali wa siasa za Tanzania.
Baada ya kusikiliza maoni ya marafiki wa mahakama ya rufaa jopo la majaji wa mahakama hiyio lililoongozwa na Jaji mkuu wa Tanzania Agostino Ramadhan limefunga rasmi kupokea hoja za pande zote mbili kati ya mkata rufani na mjibu rufani.
Umuzi wa rufani hiyo unatarajiwa kutolewa katika siku itakayotangazwa na mahakama hiyo ya rufani.
Akizungumza na VOA Mchungaji Mtikila amesema iwapo hukumu ya mgombea binafsi itasimama Tanzania itaanza kuona mwanga mpya wa kupanuka demokrasia zaidi na kuondoa ukiritimba wa vyama katika uchaguzi……Awali marafiki wa mahakama ya rufaa waliotoa maoni yao wamepinga mahakama kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam kama ilikuwa sahihi kutoa hukumu ya kushiriki kwa mgombea binafsi katika uchaguzi.

No comments:

Post a Comment