I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, April 13, 2010

SEMBE BOVU LAZUIWA KUINGIA ZANZIBAR


Zaidi ya robo tani ya unga wa sembe aina ya Jembe kutoka nchini Kenya umezuiliwa kusambazwa Zanzibar baada ya kubainika kuwa haufai kwa matumizi ya binadamu.
Mrajisi wa bodi ya chakula, dawa na vipodizi Zanzibar Dr. Burha Othaman Simai amesema sembe hilo limeingia nchini bila ya kusajiliwa na inasadikiwa limeshushwa katika bandari isiyo rasmi.
Aidha bodi hiyo imebaini kuuzwa kwa vipodozi vilivyopiwa marufuku na kuwataka wananchi kuwa wangalifu wanaponunua bidha hizo ili kuepukana na madhara

No comments:

Post a Comment