I made this widget at MyFlashFetish.com.

Friday, April 9, 2010

MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI TAIFA RAIS JAKAYA KIKWETE AMESEMA

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi taifa rais Jakaya Kikwete amesema njia zilizobuniwa na chama hicho za kukusanya fedha za kugharamia uchaguzi kwa wagombea wake hazitakiuka sheria ya gharama za uchaguzi aliyoitia saini hivi karibuni.
Amesema fedha hizo zitakazochangwa na wana CCM matumizi yake yatakuwa wazi kwa kila mgombea wakati wa kampeni ili kuona sheria ya gharama za uchaguzi haikiukwi.
Akizungumza katika uzinduzi wa mfuko wa gharama za uchaguzi kwa CCM mjini Dar es Salaam rais Kikwete amewataka wanachama, wafuasi na wapenzi wa chama hicho kujitokeza kwa wingi kuchangia mfuko huo kupitia simu za mkononi…
Aidha mwenyekiti huyo amesema fedha hizo shilingi bilioni 40 sio kwa ajili ya uchaguzi wa urais pekee bali pia zitatumika kwa wagombea wa ubunge, uwakilishi na udiwani kupitia chama hicho.Mwenyekiti huyo pia amewataka wana CCM waliojiandikisha kupiga kura kujiorodhesha katika daftari la chama hicho ili kujua idadi ya wapiga kura wake.
Chama cha Mapinduzi CCM kinatarajia kutumia zaidi ya shilingi bilioni 40 kuendeshea kampeni zake za uchaguzi kwa wagombea wa urais, uwakilishi, ububnge na udiwani kwa nchi nzima.
Katika kampeni hizo chama cha CCM kinatarajia kunua gari 26 na kuzigawa kwa kila mkoa zitakazosaidia kuendeshea kampeni kwa wagombea wake.
Hotuba ya uzinduzi huo wa uchangiaji uliofanywa na rais Kikwete usiku huu imetangazwa moja kwa moja kupitia hapa Zenji fm.

No comments:

Post a Comment