I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, April 28, 2010

ZANZIBAR


Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Zanzibar imesema maradhi yasiyo ya kuambukiza yamezidi kuongeza hapa nchini kutokana na mabadiliko ya mfumo wa maisha hapa Zanzibar.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Tiba na mratibu wa maradhi yasiyoambukiza wa wizara ya Afya na ustawi wa jamii Zanzibar Dr.Abdalla Juma Mabodi akizungumza katika warsha yakujadili namna ya kujinga na kuzuiya maradhi hayo iliyofanyika Manson Hotel mjini Zanzibar .
Dr.Mabodi amesema maradhi yasiyokuwa ya kuambukiza kama sindikizo la damu Kansa, Kisukari, Kiharusi, maradhi ambayo yameibuka kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa ambayo huleta athari katika mwili na kusababisha maradhi hayo……
Aidha amesema maradhi ya kuambukiza kwa hapa Zanzibar yamepungua kwa kiasi kikubwa na kujitokeza kwa kasi maradhi yasiyoambukiza ambayo huleta maafa na vifo.
Mkutano huo umeshirikisha wajumbe kutoka nchi mbali mbali za Afrika ikiwa Zanzibar ni mwenyeji wa mkutano huo.

No comments:

Post a Comment