I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, April 14, 2010

MVUA ZALETA ATHARI ZANZIBAR


Mvua za masika zimeanza kunyesha nchini na kuathiri baadhi ya maeneo mbali mbali na hatimaye wananchi wengine kukosa makaazi.
Kutokana na maafa hayo na mengine Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeanzisha kitengo mahsusi cha maafa ambacho kipo chini ya Ofisi ya Waziri Kiongozi.
Tukiachana na suala la mvua maafa mengine mbali mbali yamewahi kutokea nchini na kitengo hicho kimekuwa mstari wa mbele kuwasaidia na kuwaelimisha wananchi juu ya madhumuni ya kitengo hicho.
Mwangaza wa Habari leo umeingia katika kitengo hicho na kutaka kufahamu tahtmini ambayo imefanyika kwa wale walioathirika na mvua zinazoendelea kunyesha hivi sasa.
Katika mazungumzo yake na Mwangaza wa Habari waziri wa nchi ofisi ya waziri kiongozi Hamza Hassan Juma ambapo kitengo cha maafa kipo katika ofisi yake amesema kuwa kwa sasa kitengo cha maafa kinafanya tathmini ya walioathirika lakini tathmini kamili itatolewa baada ya mvua hizi za masika kumalizika...Bonyeza HAPA kumsikia Mhe HAMZA AKIZUNGUMZIA ATHARI ZA MVUA

No comments:

Post a Comment