I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, April 12, 2010

TATIZO L A MAFUTA ZANZIBAR

Idara ya nishati na madini Zanzibar imesema ukosefu wa vifaa vya kuchunguzia ubora wa mafuta ya petroli, na Dizeli kunachangia kuingia kwa nishati hiyo chini ya kiwango kinachokubalika.
Mkurugenzi wa idara hiyo bwana Zuberi amesema hali hiyo inaleta usumbufu kwa wateja wanatumia mafuta hayo.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar amesema baada ya kukosekana kwa vifaa hivyo kigezo kikubwa kinachotumika ni makisio yanayotokana na nyaraka za kusafirishia nishati hiyo.
Tatizo hilo limejitokeza baada ya madereva mbali mbali wanaoendesha vyombo vya moto kulalamika kuwa mafuta yanayoingia nchini hayako katika kiwango bora na kusababisha vyombo hivyo kuharibika haraka.
Mkurugenzi huyo amefahamisha kwa upande wa Tanzania bara wanayo maaabara ya aina hiyo kupitia Shirika la TBS ambapo wafanyabiashara wanaoingiza mafuta chini ya kiwango huchukuliwa hatua za kisheria.
Hivyo amesema Zanzibar inahitaji kuwa na vifaa hivyo ili kuwalinda watumiaji wa nishati hizo.

No comments:

Post a Comment