I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, April 29, 2010

BANK YA BODEA YAZIDI KUTOA MSAADA KWA ZANZIBAR


Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika BADEA na Mfuko wa Saudi Arabia zimeahidi kuendelea kuisaidia Zanzibar katika ujenzi wa miundombinu ya barabara na mategenezo ya uwanja wa ndege wa Pemba.
Uongozi wa taasisi hizo za kifedha umetoa ahadi hizo ulipokuwa na mazungumzo na rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Amani Abeid Karume, Ikulu mjini Zanzibar.
Katika mazungumzo hayo uongozi huo ulieleza kuwa tayari barabara zote tatu za Pemba zikiwemo barabara ya Wete-Gando, Wete-Konde na Chake -Wete ambazo wanazigharami zimo katika mpango wa ujenzi.
Aidha, taasisi hizo pia zimeelezea nia yao ya kugharamia ujenzi wa barabara za Mwera-Pogwe-Jumbi, Cheju-Unguja Ukuu na Miwani-Kizimbani.
Nae rais Karume amesem serikali katika kuimarisha sekta ya mawasiliano ikiwemo miundombinu ya barabara pia, imeweka mikakati ya kuimarisha sekta ya kilimo hasa cha umwagiliaji maji.

Benki ya BADEA inaendelea kusaidia ujenzi wa majengo mapya ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA huko Tunguu wilaya ya Kati ambapo kukamilka kwa ujenzi huo kutasaidia kuimarisha sekta ya elimu nchini

No comments:

Post a Comment