I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, April 28, 2010

18 WAFARIKI DUNIA HAPO HAPO AJALI YA GARI (TANGA)


Watu 18 wamefariki dunia papo hapo na wengine 125 wamejeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kupinduka katika eneo la Mabanda ya Papa mjini Tanga.
Basi hilo lilikuwa limebeba wanafunzi wa chuo cha kiislamu Shamsu Maarifa waliokuwa wakisafiri kwa Lori aina ya Fuso lenye namba za usajili T.757 BDB.
Kwa mujibu wa Daktari mkuu wa hospitali ya Bomba Mkoani Tanga amesema majeruhi watatu kati ya 125 hali zao ni mbaya na wanafanyiwa taratibu ya kupelekwa katika hospitali ya Mifupa ya Moi Muhimbili Jijini Dar es salaam.
Nae kaimu kamanda wa jeshi la Polisi Mkoani humo Adofsina Kapusi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo ameeleza taarifa zimesema kwamba chanzo cha ajali hiyo inatokana na mwendo wa kasi…
Hadi sasa maiti tisa zimeshatambuliwa na jamaa zao ambapo mazishi ya maiti hizo yamefanyika katika chuo hicho cha Shamsu Maarifa

No comments:

Post a Comment