I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, April 12, 2010

BEI YA SUKARI YAZIDI KUPANDA ZANZIBAR


Bei ya sukari bado Zanzibar imeonekana kuwa juu licha ahadi zilizotolewa na maafisa wa idara ya biashara Zanzibar kulipatia ufumbuzi tatizo hilo la kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo.
Kwa mujibu wa mwandishi wetu alietembelea soko kuu la mjini Chakechake Pemba kilo moja ya sukari inauzwa kati ya shilingi elfu moja na 500 hadi elfu moja na 600.
Aidha katika maduka ya reja reja ya manispaa ya mji wa Zanzibar na maeneo ya karibu kilo moja ya suakari inauzwa kati ya shilingi elfu moja na 400 hadi elfu moja na 500.
Hivi karibuni uongozi wa idara ya biashara Zanzibar umeimbia Zenji Fm radio kwamba kupanda kwa bei ya sukari kunatokana na uzalishaji mdogo wa bidhaa hiyo pamoja na kupanda bei katika soko la dunia.
Bidhaa nyingine kama vile unga wa ngano uko katika bei ya wastani ya shilingi 800 kwa kilo, lakini kilo moja ya mchele wa kawaida inauzwa kati ya shilingi 900 hadi elfu moja wakati mchele wa Mbeya unauzwa kati ya shilingi elfu moja na 300 hadi elfu moja na 500.

1 comment:

  1. Abaa sasa mwataka tuuuwaaaa . Maana sukari wallahi hainunuliki..

    ReplyDelete