I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, September 15, 2010

CUF YAZINDUA ILANI YAKE YA UCHAGUZI YA MWAKA 2010 ZANZIBAR

Chama cha wananchi CUF kimesema kitaangalia upya mambo yaliongezwa katika orodha ya mambo ya muungano baada ya makubaliano ya awali ya mwaka 1964 yaliounda muungano huo endapo kitapewa ridhaa ya kuongoza Zanzibar.

Mgombea wa urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Seif Sharif Hamad amesema mambo hayo yatajadiliwa kwa kina na uwazi ili kuhakikisha muungano huo unazifaidisha nchi zote mbili kwa msingi ya usawa.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010 ya chama hicho amesema serikali yake pia itawasiliana na serikali ya muungano kutaka kuandika katiba mpya itakayokidhi makubaliano ya muungano ya mwaka 1964 yenye muundo wa serikali tatu

Kuhusu maendeleo ya uchumi Hamad amesema serikali atakayoiunda itajenga uchumi imara kwa kuzingatia mfumo wa soko huria unatoa fursa ya ushiriki wa wananchi wote ili kuona hali zao za kimaisha zinaimarika.

Amesema sekta za kilimo, utalii, biashara, viwanda na uvuvi zitapewa umuhimu katika ujenzi wa uchumi wa kisasa pamoja na kuhakikisha matumizi bora ya raslimali ziliopo ikiwemo uchimbaji wa mafuta.

Hamad amesema serikali yake itaanzisha shirika la ndege kwa njia ya ubia na wewekezaji wa ndani na nje ili kuwa na njia za uhakika za kuinganisha Zanzibar kibiashara na kiuchumi na nchi nyingine duniani.

Amesema atafanya mazungumzo na mashirika ya kimataifa ya usafiri wa anga kuanzisha usafiri wa moja kwa moja kati ya miji mikuu yao na Zanzibar ili kuimarisha shughuli kiuchumi na biashara…

Kuhusu utumishi wa umma Hamad amesema serikali yake itapandisha mishahara ili iweze kukidhi gharama za maisha na kuhakikisha inatolewa kila baada ya wiki mbili na ambapo kima cha chini kitaanzia shilingi laki moja na nusu.

Amesema licha ya serikali kuwa na wafanyakazi wengi wasiokuwa na tija serikalini, serikali yake itakuwa na mpango maalum wa mashauriano ya kutoa maamuzi baadhi ya wafanyakazi ambao hawana tija serikalini waondolewe.

Amesema wafanyakazi hao watejengewa mazingira mazuri ya kuwa na ajira mbadala ili kuweza kuzalisha au kutoa huduma zenye tija zitakazomuwezehsa kupata mapato makubwa kuliko alivyokuwa serikalini.

1 comment:

  1. hello my friend! warm greeting ^^!
    your blog looks nice 0_0

    by the way,
    if you need to find unique typography, you can go to our website.

    best regards;

    ReplyDelete